Simba achezea kichapo Morocco
TIMU ya Simba ikiwa ugenini nchini Morocco imekubali kupokea kipigo cha bao 2-0 kutoka kwa RS Berkane ya nchini humo.
Mechi hiyo ya kombe la Shirikisho Barani Afrika imepigwa leo Jumapili katik dimba la RS Berkane. Ilikuwa mechi ya kisasi kwa kocha wa Berkane, Florence Ibenge ambaye amekuwa akishindwa kufurukuta akiwa As Vita ya Congo.
Pia ilikuwa mechi ya timu ambazo ni marafiki na zenyewe wachezaji baadhi wanaofahamiana akiwemo Tuisila Kisinda aliyewahi kuichezea Yanga. Mabao ya Berkane yamefungwa na Adama Ba dakika ya 32 na El Bahir dakika ya 41 ya mchezo huo.
Msimamo wa Kundi D baada ya Simba SC kupoteza kwa kufungwa 2-0 dhidi ya Berkane na USG kupata ushindi wa 2-0 dhidi ya Asec Mimosa. Mechi ya marejeano ya Simba na Berkane itapigwa Machi 13, mwaka huu katika dimba la Mkapa Dar.