The House of Favourite Newspapers

Simba Mama Lao Yaipiga Yanga Princess 3-0 (Picha +Video)

0

SIMBA Queens imepania kuhakikisha inatwaa ubingwa kwa mara ya pili mfululizo baada ya jana kuwabanjua Yanga Princess kwa mabao 3-0 na kukaa kileleni kwa tofauti ya pointi moja katika mchezo wa Ligi Kuu ya Wanawake Bara.

 

Yanga Princess waliongoza ligi kwa kipindi kirefu kabla ya jana kushushwa na Simba ambayo ndiyo timu ya kwanza kuifunga Yanga msimu huu.

Simba ikicheza kwa kujiamini, iliandika bao lake la kwanza kupitia kwa mchezaji mkongwe, Mwanahamisi Omary ‘Gaucho’ katika dakika ya 29 kwa shuti kali nje kidogo ya 18.

Baada ya bao hilo kuingia, Simba waliendelea kushambulia lango la Yanga ambao walionekana kutokuwa na maelewano hasa eneo la kiungo na ulinzi, dakika ya 42 walijikuta wakipunguzwa baada ya Neema Charles kutolewa kwa kadi nyekundu kutokana na kuushika mpira akiwa ndani ya 18.

 

Penalti hiyo ilipigwa kiufundi Opa Clement na kuifanya Simba iende mapumziko ikiongoza kwa mabao 2-0.Kipindi cha pili kama kawa Simba waliingia wakiwa na moto uleule na kufanikiwa kupata bao la tatu dakika ya 50 kupitia kwa mshambuliaji Mrundi, Joele Bukuru

Leave A Reply