The House of Favourite Newspapers

Simba Mdomoni Mwa Waarabu

0

MABINGWA wa Tanzania Bara, Simba wanaweza kukutana na timu kutoka Uarabuni katika hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

 

Droo ya michuano hiyo mikubwa Afrika imepangwa kufanyika Aprili 30, mwaka huu itakayochezeshwa na Shirikisho la Soka Afrika (Caf).

 

Simba imefanikiwa kufuzu hatua ya makundi ikiwa kileleni ikiwa na pointi 13 ikiwa imeweka rekodi huku ikiruhusu mabao mawili pekee na kufunga tisa katika mechi sita ilizocheza.

 

Simba inaweza kukutana na moja kati ya hizi timu tatu ambazo ni CR Belouizdad, MC Alger zote za Algeria au Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini, ambazo hizo zote zimemaliza michuano hiyo katika nafasi ya pili zikitoka kundi B, D na C, mtawalia.

Simba itaanzia ugenini katika mchezo wa kwanza wa robo fainali kati ya Mei 14-15, mwaka huu na itamalizia nyumbani katika mchezo wa pili.Klabu nane zilizofuzu hatua ya robo ni Simba, Al Ahly, Mamelodi Sundowns, CR Belouizdad, Wydad AC, Kaizer Chiefs, Esperance na MC Alger.

 

Akizungumzia hilo Kocha Mkuu wa Simba, Mfaransa, Didier Gomes, alisema: “Sisi tupo vitani, hivyo ni lazima tupambane kuhakikisha tunashinda kwa timu yoyote tutakayokutana nayo.

“Ninashukuru tumemaliza salama michuano hii bila majeruhi yeyote na hivi sasa nguvu zetu tunazielekeza katika hatua ya fobo fainali tuliyofuzu.”

STORI: WILBERT MOLANDI, Dar es Salaam

Leave A Reply