Simba SC Yaibadilishia Mbinu Yanga SC
ZIKIWA zimebaki siku 14 kabla ya watani wa jadi Yanga na Simba kukutana Oktoba 18, Simba imesema kuwa itatumia mtindo wa zigzag kupata ushindi mbele ya watani zao wa jadi.
Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Sven Vandenbroeck, jana Oktoba 4 iliwachapa na wanajeshi kamili JKT Tanzania bao 4-0, sasa watakutana na Yanga, Oktoba 18.
Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara alisema; “Tumemaliza kupiga ule mpira wetu mbele ya JKT Tanzania, sasa tunarudi kujiweka sawa kwa ajili ya mechi yetu dhidi ya Yanga, ratiba imebadilika kidogo kutokana na ratiba ya mechi ya timu ya Taifa ya Tanzania ila tupo tayari tutakuja na kitu kinaitwa zigzag tunaamini tutashinda,” alisema Manara.
Lunyamadzo Mlyuka, Dares Salaam