The House of Favourite Newspapers

Simba Wamlilia Shabiki Wao Aliyejinyonga

0

Baada ya Taarifa kusambaa kuwa Kijana Khalfan Mwambena (17) mkazi wa Jijini Mbeya na Shabiki kindaki ndaki wa Simba kusambaa kuwa amejiua baada ya Simba kupoteza mchezo dhidi ya Mbeya City.

 

Klabu ya Simba Kupitia Meneja wa Habari na mawasiliano wa Klabu hiyo, Ahmed Ally umekanusha taarifa hiyo na kueleza kuwa Shabiki huyo amefariki siku ya mchezo huo majira ya asubuhi kabla hata ya mchezo kuchezwa.

 

Sasa klabu ya Simba imekwenda mbali na kuthamini mapenzi ya Shabiki huyo kwa Klabu ya Simba. Simba imetoa taarifa kuonesha kuguswa na msiba wa shabiki huyo na kutoa pole kwa familia na Wanasimba kwa ujumla.

 

Tazama sehemu ya Taarifa ya Simba kwenda kwa Familia, Wapenzi, Wanachama na Mashabiki.

Leave A Reply