The House of Favourite Newspapers

Simba waponda mazoezi ya Yanga

0

MASHABIKI wa Simba wameyabeza mazoezi ya Yanga kwa kusema ni ya kawaida na kamwe wasijidanganye kama yatawawezesha kuifunga timu yao.

Mmoja wa wapenzi wa Simba kisiwani hapa, Ali Yussuf aliliambia Championi Jumamosi kuwa, Yanga inayonolewa na Kocha Hans van Der Pluijm siyo timu ya kuitisha Simba, badala yake wanapaswa kurudisha kwanza kipigo cha mabao 5-0 walichokipata mwaka 2012.

“Nimetazama mazoezi haya ya Yanga lakini nakuambia haitaweza kufanya lolote kwa Simba, wana kazi kubwa ya kurudisha zile bao 5-0 tulizowafunga,” alisema Yussuf.

Shabiki mwingine aliyefahamika kwa jina la Mbwana Amour, alisema anaamini timu yao ya Simba haipo vizuri lakini amepata faraja na mazoezi ya Yanga kwani ni ya kawaida sana.

“Kwa mazoezi haya ya Yanga, nadhani hata kama Simba ipo vibaya kama ilivyo haiwezi kufungwa, ni ya kawaida mno,” alisema Amour. Yanga iliondoka Pemba, jana Ijumaa kurejea Dar es Salaam tayari kwa mchezo wa leo dhidi ya Simba kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

JIUNGE NA VODACOM MICHEZO KIGANJANI.

CHAMPIONI

Leave A Reply