The House of Favourite Newspapers

Simba Yailaza Kagera Sugar Kaitaba, Yaichapa 2-0

0

 

TIMU ya Simba imeendeleza wimbi la ushindi kwenye mfululizo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara baada ya leo Aprili 21 kuinyanyasa Kagera Sugar kwa kuilaza kwa magoli 2-0 mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera.

 

Magoli ya wekundu wa msimbazi Simba yalipatikana kwenye kipindi cha kwanza kuptia kwa Luis Miquissone dakika ya 13’ na Chris Mushimba Mugalu dakika ya 23’.

 

Baada ya mchezo kocha msaidizi wa Simba Suleiman Matola amesema kipindi cha pili waliingia na mbinu ya kupoza mchezo kwa ili wasiwachoshe wachezaji wao kwa sababu ya mechi nyingi zinazokuja ambazo zimefuatana.

Katika matokeo ya mechi zilizochezwa leo nyingine Ruvu Shooting  wamechopoza na ushindi mzito wa mabao 5-1 dhidi ya Mwadui Fc Polisi Tanzania wakiwa uwanja nyumbani wamefungwa  1-0 na Mbeya City.

 

Kwa matokeo hayo Simba imefikisha alama 55, ikicheza mechi 23 na Yanga wanaongoza ligi kwa alama 57 wakicheza michezo 26.

 

Leave A Reply