The House of Favourite Newspapers

Simba yaionyesha Yanga kufuru Mwanza

UKISIKIA kipyenga kimelia ndani ya CCM Kirumba leo jioni, Simba itakuwa imeshatibua mambo kwenye maskani hiyo ya Yanga. Simba itakipiga na KMC kwenye mechi ya ligi katika Uwanja huo, hiyo ikiwa ni mechi ya tatu ya Mnyama ya ligi kwenye nyasi hizo msimu huu.

 

Sasa basi, takwimu za mapato kwenye mechi za ligi za hivikaribuni katika uwanja huo ambao Yanga inautumia kama nyumbani, ziko vizuri kwa Simba.

 

Kwa mujibu wa vyanzo vya uhakika ndani ya Chama cha Soka cha Mwanza, Simba kwenye mechi zake mbili tu dhidi ya Mbao na Alliance imeingiza Sh.96.6 dhidi ya 119.1 walizoingiza Yanga kwenye mechi tano.

 

Hiyo inamaanisha kwamba, Yanga ikiingiza na mapato ya leo dhidi ya KMC itawafunika Yanga kwani makadirio yanaonyesha mapato yake kwenye uwanja huo si chini ya Sh.Mil 40.

 

Kwenye mechi na Alliance waliingiza Sh.Mil 45.8 na Mbao Sh.Mil 50.7. Mechi ya Yanga; dhidi ya Kagera Sh.Mil 9.8,

Lyon Sh.Mil 7.9, Alliance Sh.Mil 38.3, Alliance Sh.Mil 27.2 na ule wa Mbao Sh.Mil 36. Hiyo ni rekodi kubwa ya mapato kwa Simba kutokea kwenye Uwanja huo katika misimu ya hivikaribuni haswa Yanga ikiutumia kama maskani yake na Uwanja wa Nyumbani. Tathmini ya Spoti Xtra imebaini kwamba Simba iliizidi Yanga kwa mashabiki kutokana na kufanya vizuri kimataifa.

Comments are closed.