The House of Favourite Newspapers

Simba Yaipiga 4G JKT Tanzania Jamhuri, Dodoma

0

KIKOSI cha Simba kinachonolewa na Kocha Mkuu, Sven Vandenbroeck, leo Oktoba 4 kimeibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya JKT Tanzania kwenye mchezo uliochezwa Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.

Mabao ya Simba yalifungwa na Meddie Kagere aliyefunga mabao mawili dakika ya 4 na dakika ya 40 na mabao mengine yalifungwa na Chris Mugalu dakika ya 6 na Luis Miquissone naye alitupia bao dakika ya 51.

Ushindi huo unaifanya Simba kufikisha jumla ya pointi 13 ikiwa nafasi ya kwanza na ina mabao 14 kibindoni huku nafasi ya pili ikiwa mikononi mwa Yanga yenye pointi 13 tofauti kwenye idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa.

Yanga imefunga jumla ya mabao 7 kibindoni na ushindi wa jana, Oktoba 3 ulikuwa ni wa kwanza kwa Yanga kushinda mabao zaidi ya mabao 3 uwanjani.

Leave A Reply