The House of Favourite Newspapers

Simba yaletewa straika zaidi ya Ngoma

0

Nicodemus Jonas, Dar es Salaam

SIMBA imeambiwa wala isiwe na papara kikifika kipindi cha usajili wa dirisha dogo kwani ikitaka italetewa straika hatari zaidi ya Donald Ngoma wa Yanga ambaye ana mabao manne katika Ligi Kuu Bara.

Aliyetamka maneno hayo ni kiungo Justice Majabvi wa Simba, ambaye ameona timu yake haina mastraika wengi uwanjani, hivyo waliopo wakiumia tu hali huwa si nzuri.

Majabvi alisema: “Kama Simba ikitaka kusajili tena, nadhani utakuwa wakati wa kutazama vipaji kutoka kwetu Zimbabwe ambako kuna wachezaji wengi wazuri.”

“Wachezaji hao wengi ni wa gharama nafuu, kuna washambuliaji wakali kuliko yule Ngoma anayeonekana anajua sana Yanga, kama viongozi wakihitaji nipo tayari kutafuta straika mkali na wachezaji wengine.”

Majabvi alisema Zimbabwe inaaminiwa kuwa na wachezaji wengi wenye vipaji, ndiyo maana wamejaa katika Ligi Kuu Afrika Kusini wakicheza soka la kulipwa.

Simba ina mastraika wanne ambao ni Hamisi Kiiza, Mussa Mgosi, Ibrahim Ajibu, Boniface Maganga na Pape N’daw.

Leave A Reply