The House of Favourite Newspapers

Simba Yapangua Benchi la Ufundi

0

Klabu ya soka ya Simba imetoa taarifa kwa umma kuwa kwa makubaliano ya pande zote mbili imeachana rasmi ba kocha wa makipa Mohamed Muharami na meneja wa timu, Patrick Rweyemamu.

 

Katika taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Idara ya Uendeshaji, Dokta Arnold Kashembe imeeleza kwamba Klabu yao imekusudia kuboresha benchi lake la ufundi, na hivi karibuni wataweka hadharani majina ya watu ambao wataziba nafasi hizo.

 

Klabu ya Simba inawatakia kila la heri kwenye maisha yao mapya watendaji hao walioondolewa. Kuondolewa kwa wawili hao kunahusishwa na matokeo mabaya ya Simba katika mechi mbili zilizopita za ligi kuu Tanzania bara dhidi ya Prisons na Ruvu Shooting ambazo walipoteza.

Leave A Reply