The House of Favourite Newspapers

Simba Yashindwa Kutinga Nusu Fainali Licha ya Ushindi wa 3-0

0

TIMU ya Simba licha ya ushindi Ilioupata wa mabao 3 – 0, dhidi ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini bado umeshindwa kuivusha kwenda hatua ya Nusu fainali baada ya kutoka kwa jumla ya mabao 5-4, mechi iliyochezwa leo Mei 22, 2021 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa.

 

Simba ambayo ilionekana moto tangu dakika ya kwanza, ilifanikiwa kupata magoli yake kupitia kwa Nahodha John Bocco alifunga mawili dakika ya 23′ na 56′ na msumari wa tatu kupitia kwa  mwamba wa Lusaka Claoutus Chama dakika ya 85.

 

Kwa matokeo hayo Kaizer Chiefs imetinga hatua ya Nusu Fainali na itakumbana na mshindi kati ya Wydad Casablanca ya Morocco anayoichezea mtanzania Simon Msuva au MC Alger ya Algeria.

 

Katika matokeo mengine Mamelodi Sundowns  yya Afrika Kusini, wametupwa nje ya michuano hiyo na mabingwa watetezi Al Ahly ya Misri baada ya kutoka sare ya 1-1 ambayo imefanya matokeo ya jumla kuwa 3-1 baada ya mechi ya mkondo wa kwanza kuisha kwa Ahly kushinda kwa 2-0.

 

Leave A Reply