The House of Favourite Newspapers

Simba Yatoa Tamko Kuhusu Ishu Ya Zimbwe Kuwekwa Rada Za Yanga

0

BAADA ya kuwa na tetesi kwamba beki wa kushoto wa Simba, Mohammed Hussein ‘Zimbwe Jr’ au ‘Tshabalala’ ameingia kwenye rada za watani wa jadi, Yanga, Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara ameomba uongozi umalizana na mchezaji huyo mapema kabla hajasepa huku akiweka wazi kwamba watamruhusu mchezaji huyo kwenda nje ya nchi na sio katika timu nyingine.

 

Ndani ya Simba, Zimbwe mkataba wake umebaki miezi miwili ambapo bado hajaongeza dili jingine licha ya kuwa kwenye mazungumzo na mabosi hao.

 

Kupitia ukurasa wa Instagrma wa Haji Manara ameandika namna hii:-“Wewe ndio mchezaji unaeimbwa zaidi na wasanii wa Bongo kwa mahaba yao kwako.

Wewe ni Captain, (nahodha) wetu unaependwa ná kila mmoja ndani ya Simba.

 

“Hii ni timu ya maisha yako na hapa ndio umekulia na kupata jina lako. Mimi na wewe tuliingia pamoja msimu wa 2014 ni mate wangu. Tumetoka mbali na hii klabu. Tunayajua mengi mazuri na changamoto za klabu hii.

 

“Tumetengeneza bond kubwa na Simba, hakuna thamani ya pesa itakayotufanya tuondoke Simba kwenda klabu nyingine ya Tanzania.

 

“Wanasimba wamenituma nikwambie hadharani, umalizane haraka na uongozi wa klabu kuhusu usajili wako na hawatakubali kukupoteza kwa namna yoyote ile. Sanasana watakuruhusu uende nje ya nchi hii.

 

“Don’t forget, (usisahau) wanaokushawishi leo walikudhihaki jana, usikubali kuiacha team ambayo inakuandaa uwe legendary wake na inayokupa furaha kisha ukacheze team usiyoishabikia eti kwa sababu ya visumuni vya kupita.

 

“Furaha na amani ya moyo inazidi rupia za kupita !Babra, (Gonzalez) boss wangu, nchi haitatuelewa Zimbwe akiondoka

“Huyu ni Mtoto wa Simba, limalize hili tuendelee kuonyesha nini Simba inadhamiria katika muendelezo wa ukubwa wake!

“Naombeni tutangeneze hashtag yoyote ya kumtaka Mohammed Hussein Zimbwe Junior aongeze mkataba Simba,” .

Leave A Reply