The House of Favourite Newspapers

Simu Mpya Kutoka Tecno, Camon C9 Yatua Dar

0
Teknolojia ya simu inaendelea kukua siku baada ya siku, baada ya simu feki kuzimwa na Mamlaka ya Mawasilinao nchini (TCRA), Tecno Mobile imetangaza kuzindua simu kali ya CAMON C9 yenye uwezo wa hali ya juu katika kupiga picha, uwezo wa 4G LTE na teknolojia mbali mbali za kisasa. Ikiwa simu yako ni miongoni mwa simu zilizofungiwa na TCRA basi ondoa shaka kwani simu hii mpya kutoka Tecno utaipata kwa gharama nafuu kabisa.
Tecno Camon C9 inaanza kuuzwa rasmi tarehe 25 Juni 2016. Unaweza kufanya manunuzi ya awali (pre-order) uwe miongoni wa Watanzania wa awali kujipatia simu hii. Kufanya manunuzi ya awali tembelea exclusive show room za Tecno jijini Dar zilizopo City Mall, Clock tower na Mobile plaza ghorofa ya pili.
Kufanya manunuzi ya awali unahitaji kufanya malipo ya awali ya Tsh. 30,000 ambapo mteja atapata kadi ya “huduma kwa wateja kutoka” Tecno na kifurushi cha zawadi (gift hamper) za bidhaa kutoka Tecno. Kadi ya huduma kwa wateja itatumika katika kutengenezewa simu katika duka zetu za Tecno baada ya kujipatia simu yenyewe.
Mauzo rasmi yanaanza 25 Juni 2016 ambapo watakao kuwa wamefanya pre-order watatakiwa kukamilisha malipo yao dukani hapo na kisha kuingizwa moja kwa moja kwenye droo ya kijishindia zawadi mbali mbali.
Zawadi za Droo
Zawadi ya Kwanza: Samsung LED TV yenye thamani ya Milioni 1.6
Zawadi ya pili: Jiko ya kutumia umeme (washindi wawili)
Zawadi ya tatu: Birika linalotumia umeme (washindi wawili)
Na zawadi zingine nyingi
Kila mteja atakaye nunua Tecno C9 Jumamosi katika First sale itakayofanyka pale City Mall (Showroom inaonekana kwenye picha) atakuwa mshindi.
Baadhi ya sifa za Camon C9 itauzwa katika maduka ya Tecno ikiwa katika rangi 3 tofauti na hizi ni baadhi ya sifa zake.
Camera ya hali ya juu
Kama mpenzi wa picha Camon C9 imekupa Camera unaihitaji kwani inaweza kutambua sura na kupiga selfie kali hata ukiwa gizani.
Pia Camera yake ina urembo wa kweli (make-up) ambayo itafanya picha zako kuwa na mvuto wa asili kitaalamu imeitwa
(Insert video)
Watu 50 ndani ya selfie moja
Inasemekana Tecno Camon C9 ina uwezo wa kujaza watu wengi kwenye selfie moja zaidi ya simu yoyote duniani. Camera ya C9 inachukua angle kubwa zaidi hivyo kukuwezesha kupata selfie nzuri hivyo kuchukua watu wengi zaidi.
Jinsi mpya ya kupiga selfie ukitumia Camera ya kati
Tecno Camon C9 itaondoa issue za selfie kutokuwa kati kwa kutumiacamera iliyo katikati ya simu ambayo wameita “The Perfect Selfie camera”
Umeshawahi kufikiria macho yanaweza kufungua simu?  Camon C9 ina Iris recognition
Sasa hutokuwa sababu ya kuweka password zinazofanana na lugha ya kirumi kwasababu Tecno imebadilisha mfumo wa namna unaweka neno la siri kwenye simu kwa kuleta teknolojia mpya ya IRIS recognition ambayo inatumia macho kufungua simu. Tecno Camon C9 inatumia teknolojia hii kumuwezesha mmliki wa simu ku-unlock simu kwa kuitizama tu.
Unaweza kutembelea kurasa za mitandao ya kijamii ya Tecno kujua zaidi
Leave A Reply