The House of Favourite Newspapers

Scene za Mapenzi Zamtesa Mwanaheri

0
Mwigizaji wa Bongo Muvi, Mwanaheri Ahmed.

 MAYASA MARIWATA, GAZETI LA AMANI, HABARI

MWIGIZAJI wa Bongo Muvi, Mwanaheri Ahmed, amefunguka kuwa, suala la kucheza ‘sini’ (scene) za kimapenzi kwenye filamu huwa linamtesa hasa linapokuja suala la kumlaghai mwanaume.

Akipiga stori na Showbiz Xtra , Mwanaheri alisema kuwa, pamoja na mwigizaji kupaswa kuvaa uhusika wa scene yoyote ile unayopangiwa, lakini kwake uhusika wa mapenzi huwa unamtesa na kumnyima usingizi.

“Scene za malavidavi kwangu huwa ni mtihani na sizipendi, huwa zinaninyima amani hasa ninapotakiwa kumlaghai mwanaume, wakati mwingine nahisi nikijibebisha sana, naweza kumkwaza baby wangu. Ila uhusika wa kukasirika hata kama utanikurupusha usingizini, nitakuwa huru nao,” alisema.

Leave A Reply