Benki ya NMB imedhibitisha uongozi na sifa yake ya kuwa taasisi kinara wa huduma za kifedha nchini na isiyo kuwa na
mpinzani, katika kulihudumia taifa baada ya kutwaa tuzo 18 za ubora za kitaifa na kimataifa.
Benki hiyo itametangaza kuwa, tuzo 10 za kimataifa imwetunukiwa hivi karibuni kwa kuwahudumia vyema wateja wake na
watanzania wote kwa ujumla, pamoja na kuwa kinara wa ujumuishaji wa kifedha nchini. Nne kati ya tuzo hizo, zimetolewa kwa
Afisa Mtendaji Mkuu wa benki hiyo, Bi. Ruth Zaipuna kwa kuwa kiongozi bora.
Akizungumza katika hafla ya kuzitangaza tuzo hizo, Bi, Ruth alizitaja baadhi ya tuzo hizo kutoka kwenye majarida ya kimataifa
zikiwa ni pamoja na:
Benki Bora Tanzania kwa mwaka 2022 – Kutoka Jarida la Global Brands Magazine
Benki Bora ya Wateja Binafsi na Biashara – Kutoka Jarida la World Economic Magazine, Jarida la International Business
Magazine na Jarida la Global Banking and Finance Review
Benki Bora katika Kilimo Biashara – Kutoka Jarida la Global Brands Magazine
Ubunifu Bora katika Huduma za Kibenki kwa Wateja Binafsi Tanzania – Kutoka International Bankers Award
Benki Bora kwa Wateja Maalum – kutoka International Bankers
Afisa Mtendaji Mkuu Bora kwa Mabenki nchini Tanzania – kutoka Jarida la World Economic Magazine, Jarida la Global
Brands Magazine na African Bank 4.0 Summit
Hatifungani Bora ya Mwaka 2022 – kutoka Mtandao wa Mitaji kwa Wajasiliamali Wadogo na wa Kati ambao
wameshirikiana na nchi za G20 na IFC.
Tuzo hizi kutoka majarida na taasisi zinazoheshimika duniani, zimeitambulisha Benki ya NMB kitaifa na kimataifa, hivyo basi,
kuitambulisha sekta na nchi yetu kimataifa. Lakini pia, zinadhihirisha imani kubwa na heshima waliyonayo sokoni.
Wz
Kwa upande wa tuzo za kitaifa, NMB ilishinda tuzo tatu za Mamlaka ya Mapato (TRA) ikiwemo ile ya Mshindi wa Jumla ya taasisi
zinazolipa kodi kubwa na kwa kuzingatia misingi na kanuni bora za ulipaji kodi.
Akizungumza kabla ya kupokea tuzo hizo, Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya NMB, Bw. Benson Mahenya, alisema benki hiyo
ina kila sababu ya kujivunia tuzo hizo, kwani ni matokeo ya kazi kubwa inayofanywa na manejimenti pamoja na wafanyakazi
wote kwa ujumla. Aliongeza kua, mafanikio hayo yametokana na ubora na viwango vya kimataifa vya huduma zote
zinazotolewa na Benki ya NMB pamoja na uendeshaji wake.