The House of Favourite Newspapers

SIRI YA VIPOCHI VYA WASANII WA WCB NI HII

WASANII wa Lebo ya Wasafi Classic Baby (WCB) wamekuwa wakionekana sehemu mbalimbali wakiwa na vipochi kiunoni huku mashabiki wao wakihoji, wanawekea nini?  

 

Ijumaa katika kufanya udadisi lilibaini kuwa, kwanza ni fasheni tu ambayo kundi hilo limeamua kuja nayo lakini vipochi hivyo vinatumika kuweka vitu vya kawaida tu kama simu, leso, pesa na vitu vingine vidogovidogo.

Mmoja wa wasanii hao, Mwajuma Abdul ‘Queen Darleen’ alisema: “Ni staili yetu tu tumeamua kuja nayo, tunaweka vitu vidogovidogo tu. Ni sawa na ile staili ya kutembea umeshika glasi ya plastiki rangi nyekundu, na unaona wengine wameiga, hata hii ya vipochi utaona wengine wanaiga.”

Stori: Richard Bukos

Comments are closed.