Snura, Ney, Stamina, Mc Kinata, Chegge Chigunda, Maua Sama Waiteka Tmk kwa Tamasha la Zege Day
WASANII mbalimbali Leo wamefanikiwa kuusimamisha ukanda wa Wilaya ya Temeke na viunga vya jirani Jijini Dar es Salaam kwa kuwakutanisha mashabiki mbalimbali kwenye tamanasha la Kimataifa lililofahamika kama ‘Zege Day’ lililofanyika kwenye viwanja vya Mwenbe Yanga
Tamasha Hilo ambalo lilinogeshwa na wasanii wenye mvuto katika miondoko mbalimbali ikiwemo singeli, bongofleva na muziki wa dansi ni pamoja na Ney wa Mitego, MC Kinata, Maua Sama, Snura Mushi na Mwanamuziki mkongwe katika Tasnia ya muziki wa dansi Josse Mara.
Mbali ya wasanii hao wengine walio amsha hisia pindi walipopanda jukwaani ni pamoja na msanii Stamina.
Huku wasanii wengine waliokonga nyoyo za mashabiki waliofika kwenye tamasha hilo la ‘Zege Day’ ni pamoja na Dayoo,Micky Singer,Rasco Sambo,Lody Music, Sir Jay, Nedy Music, Kayumba, Mzee wa Bwax na Sholomwamba
Akizungumza na Waandishi wa Habari wakati Tamasha Hilo likiendelea mmoja wa viongozi wa Kampuni ya Clouds Media Group (MMG) Sebastian Maganga alilielezea Tamasha Hilo la Zege Day kwa kusema
kuwa ni la Kimataifa na linafanyika duniani kote hivyo wao MMG wameratibu ikiwa ni katika kutambua na kuthamini mchango wa vijana wauza Chips kwa kuwarahisishia wakaazi katika maeneo mbalimbali kupata chakula cha haraka.
” Sote tunajua kuwa maisha ya kimjini yanaratiba ndefu na pana na hapo ndipo utamaduni wa Zege ulipoanzia sisi kama Clouds tumejikita katika kutoa ajira kwa vijana ndipo tulipokaa na kukubaliana kuja kufanya Tamasha hili hapa Mwembe Yanga baada ya wapenda Zege lialia kupiga kura” alisema Maganga.
Maganga aliongeza kwa kusema kuwa hakuna historia kamili wapi ilikoanzia Chips Zege lakini historia inasema kuwa watanzania wenye asili ya Bara la Asia ndiyo walianza kuuza Chip’s maeneo ya Ilala Jijini Dar es Salaam na baadaye chakula hicho kikajizolea umaarufu.
Aidha Maganga amewashukuru wadhamini wa Tamasha Hilo ambao ni kinywaji baridi cha Pepsi,The Kick na wazalishaji wa sausages.