SPORT XTRA LAZIDI KUJIIMARISHA KWA WASOMAJI
KIKOSI cha mauzo cha kampuni ya Global Publishers Ltd (GPL) watoaji wa magazeti ya Uwazi, Ijumaa, Ijumaa Wikienda, Risasi, Championi na Spoti Xtra, leo Jumapili kimeingia tena mitaani na kuwafikishia wasomaji gazeti maarufu nchini la michezo na burudani, Spoti Xtra, ambapo walionekana kuligombea baada ya kuanza kulizoea kwa habari zake motomoto, zikiwemo makala za burudani, michezo, hadithi za kusisimua na katuni.
Wasomaji hao wameomba magazeti hayo yasambazwe kwa wingi sehemu mbalimbali ili waweze kuyapata kwa urahisi. Leo kikosi hicho kilitembelea maeneo ya Mbagala-Zakhem, Charambe, Kizuiani Vikindu na kwengine.
Matukio katika picha:
Mama-lishe akijipatia gazeti pendwa la michezo la Spot Xtra.
Wasomaji wa Mbagala-Zakhem na Vikindu walivyolichangamkia Spoti Xtra leo.
PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS
Comments are closed.