KAMPUNI ya kubashiri matokeo ya SportPesa imeikabidhi Kampuni ya Global Publishers kupitia Gazeti la Championi tuzo kutokana na ushirikiano mzuri ambao wamekuwa nao.
SportPesa imeikabidhi Global Publishers tuzo hiyo leo ikishukuru kutokana na ushirikiano mzuri ambao kupitia Gazeti la Championi ilionyesha kwa kampuni hiyo mara baada ya timu ya Everton kutua hapa nchini mwezi Julai.
“Tunashukuru kwa ushirikiano wenu kuanzia tulipoanza kufanya kazi nanyi, lakini pia mlituonyesha ushirikiano mzuri sana wakati timu ya Everton ilipotua hapa nchini kucheza na Gor Mahia,” alisema Ofisa Uhusiano wa Sportpesa Sabrina Msuya.
PICHA NA ABEID LIJEY | GPL