SPOTI XTRA LAZIDI KUWASHIKA MTAANI – VIDEO
TIMU-kazi ya wachapishaji wa gazeti la SPOTI XTRA, mapema leo imezama tena mitaa mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam kwa ajili ya kulinadi gazeti hilo ambalo lilikuwa likitoka mara moja kwa wiki na sasa linatoka mara mbili kwa maana ya siku ya Alhamisi na Jumapili kwa bei ya shilingi 500.
Gazeti hili linalochapishwa na Kampuni ya Global Publishers Ltd, limeendelea kuwashika vilivyo wasomaji wake mbalimbali kiasi cha kuutaka uongozi uzidishe zaidi usambazaji wake ili liwafikie watu wengi, tofauti na lilivyo sasa ambapo limekuwa likinunuliwa na kuisha kabisa huku likiwaacha baadhi yao na kiu ya kulisoma.
Akizungumzia ujio huo wa gazeti hilo la Spoti Xtra kila Alhamisi, Mrisho amesema lengo kubwa ni kumaliza kiu ya wapenzi wa habari za michezo na ndiyo sababu kubwa ya kuliingiza mtaani Alhamisi na Jumapili.
Spoti Xtra limesheheni takwimu za soka na michezo mbalimbali inayopendwa duniani, uchambuzi makini wa mechi na masuala ya michezo bila kusahau ratiba na matokeo ya ligi zote kubwa duniani.
Aidha, Spoti Xtra limesheheni makala za kuvutia za michezo, stori za burudani na mastaa wa ndani na nje ya nchi.
Unaambiwa kwamba, Spoti Xtra linakupa uhondo zaidi kwa #Jero, pia linakupa fursa ya kushinda zawadi kibao zikiwemo jezi orijino za timu za Ulaya uzipendazo.
Picha zote hizi zinaonyesha baadhi ya wafanyakazi wa gazeti la SPOTI XTRA wakiwa katika mitaa ya Makumbusho, Morocco, Magomeni na Karume, Ilala tayari kulinadi gazeti hilo ambalo wasomaji wake wamelipenda na kuendelea kuahidi kulisoma kila siku ya Alhamisi na Jumapili linapoingia mitaani.
PICHA NA DENIS MTIMA | GPL
Comments are closed.