The House of Favourite Newspapers

Straika Simba: Yanga Msilete Timu Uwanjani

0

STRAIKA wa zamani wa Simba ambaye kwa sasa anakinoa kikosi cha Simba Queens, Mussa Hassan ‘Mgosi’ amewaonya Yanga kuwa wasiingize timu uwanjani kwani watakumbana na kipigo cha aibu.

 

Mgosi alisema ukiwatazama Yanga hawana uwezo hata robo wa kuweza kuwafunga Simba na badala yake watakwenda kukutana na kipigo cha aibu na ili kuliepuka hilo ni vema wakabaki kambini tu na Simba wachukue pointi za mezani.

Akizungumza na Championi Jumamosi, Mgosi alisema Yanga ni kama wanajisumbua kutaka kushindana na Simba kwa sasa kwa sababu hawana wachezaji bora na wanatakiwa wakae kwa miaka mitano ndiyo kidogo wanaweza wakapata timu ya kuweza kushindana na Simba.

 

“Mimi nawaambia Yanga kama itawapendeza wasipeleke timu uwanjani, kwa sababu kitakachokwenda kuwakuta ni aibu kwao, sasa ili waepuke hiyo aibu wabaki tu Kigamboni (walikoweka kambi) na Simba wachukue pointi tatu kwa sababu timu hawana, labda baada ya miaka mitano mbele huko,” alisema Mgosi.

STORI: ISSA LIPONDA, Dar es Salaam

Leave A Reply