STRESS ZA IDRISS, WEMA AAMUA KUJILIWAZA KWA PICHA HIZI
STRESS za kununiwa na Idriss Sultan, zinaendelea kumtesa Diva kutoka kiwanda cha Bongo muvi, Wema Sepetu, ambaye hivi karibuni ameamua kujiliwaza kwa picha nzuri, kwani licha ya kumuomba msamaha kupitia ukurasa wake wa Instagram, X- wake huyo bado hataki kumsamehe.
Kupitia picha hizo zenye mvuto wa hali ya juu Wema
Ameziambatanisha na ujumbe tofauti tofauti.
“Haikuwa kusudio langu”
“Wa kunizima hajazaliwa bado jamani… halafu mjue kutofautisha kati ya kujaaliwa na kujitakia… nyingi kwa maulana wangu… Sikujitakia ni majaaliwa tu” ameandika Wema.
Kitendo cha Wema kutohudhuria kwenye uzinduzi wa viatu vyake ndiyo haswa kilichomkasirisha Idriss , ambaye yeye alimsapoti kwa kiasi kikubwa kwenye uzinduzi wa filamu yake mpya ya Heaven Sent.
NA ISRI MOHAMED/GPL