The House of Favourite Newspapers

Suarez Amwaga Machozi Atletico Ikifuzu Uefa

0

ATLETICO Madrid ilibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Porto na kufanikiwa kufuzu kwenda hatua ya 16 bora
ya Ligi ya Mabingwa
Ulaya huku staa wake Luis Suarez alimwaga machozi baada ya kuumia na kutolewauwanjani.
Atletico
ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 kwenye mchezo ambao ulipigwa katika Uwanja wa Do Dragão, Porto.


Katika mchezo
huo, Suarez ambaye alianza kisha alitolewa dakika ya 13 ya mchezo baada ya kuumia na akienda
benchi huku akimwaga machozi.


Timu hiyo ilikuwa katika Kundi B la
kifo ambalo lilikuwa na timu za Liverpool, Porto, AC Milan na Atletico wenyewe.
Liverpool na Atletico ndiyo
wamefuzu kwenda 16 bora, huku Porto wao wakielekea Europa League na Milan
atolewa kwenye
michuano hiyo.


Katika mechi za
juzi, pia RB Leipzig ambayo ilikuwa Kundi A ilifanikiwa kufuzu kwenda Europa League.
Na timu nyingine
ambayo imetoka ni Club Brugge, Besiktas na Shakhtar Donetsk

Leave A Reply