Taifa Stars Yaichapa Namibia, Yafufua Matumaini CHAN
TAIFA Stars jana imefanikiwa kupata ushindi wake wa kwanza kwenye michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani (CHAN) inayofanyika nchini Cameroon.
Bao pekee la Farid Mussa Malik dakika ya 65 limetosha kuipa Tanzania ushindi wa 1-0 dhidi ya Namibia katika mchezo wa Kundi D.
Kwa ushindi huo, Tanzania inafufua matumaini ya kwenda Robo Fainali iwapo itashinda mechi ya mwisho dhidi ya Guinea Jumatano.
Baada ya sare ya 1-1 katika michezo uliotangulia jana jioni, sasa Guinea na Zambia zinalingana kwa pointi, nne kila timu zikifuatiwa na Tanzania yenye pointi tatu, wakati Namibia imeaga mashindano baada ya kufungwa mechi zote mbili za mwanzo.