Takwimu za Chama Simba ni Balaa
TANGU ajiunge na timu ya Simba, Septemba 15, 2019, Clatous Chama raia wa Zambia amecheza jumla ya michezo 111, na kuwa na mchango mkubwa katika kikosi hicho.
Kiungo huyo mchezeshaji amekuwa na umuhimu mkubwa katika kikosi cha Simba kuanzia katika michuano ya ndani ya Tanzania na ile ya Kimataifa, akiwa msaada katika kubeba mataji ya Ligi Kuu Bara na Kombe la FA.
Baada ya juzi kutoa asisti ya bao lililofungwa na Luis Miquissone katika mchezo wa ushindi wa mabao 0-2 dhidi ya Kagera Sugar, amefanikisha kufi kisha asisti 45 tangu ajiunge na Simba akitokea Power Dynamos ya Zambia.
Kwa msimu huu mpaka sasa katika Ligi Kuu Bara, Chama ameshafi kisha jumla ya asisti 11 na bado zimesalia mechi kadhaa.Katika mabao Chama amefunga jumla ya mabao 30 kwenye michezo yote ikiwemo ile ya Ligi ya Mabingwa ambayo kwa msimu huu Simba imeingia hatua ya robo fainali.
STORI NA LEENE ESSAU | GPL