The House of Favourite Newspapers

Tambo za wachezaji, Makocha Yanga, Simba Ngao Ya Jamii

0
Mshambiliaji wa Simba Haruna Niyonzima.

 

MIAMBA ya soka nch­ini, Simba na Yanga, inatarajia kukutana leo Juma­tano katika Uwanja wa Taifa, Da es Sa­laam kuondoa ubi­shi unaoendelea kwa sasa.

Mchezo huu ni wa Ngao ya Jamii ambao u n a a s h i r i a kuanza kwa msimu mpya wa ligi kuu, i n a y o t a r a ­jiwa kuanza k u t i m u a vumbi Ago­sti 26 kwa timu 16 k u s h u k a dimbani.

Championi Ju­m a t a n o l i n a k u letea tambo mbalimbali za wachezaji na m a kocha kuelek e a m c h ­ezo huo u t a k a ­oanza ku­p i g w a saa 10:00 jioni leo.

SHIZA KICHUYA

“Tumejiandaa vizuri na mchezo huo kwa kuwa kikosi chetu kipo vizuri na tuna­hitaji kushinda.

“Kwa upande wa wachezaji hatuna mchezaji atakayetusumbua katika mchezo huo zaidi ya Ibrahim Ajibu ambaye ki­wango chake tunakifahamu vizuri hakuna asiyekijua.”

Kikosi cha timu ya Yanga.

HARUNA NIYONZIMA

“Siku zote mechi ya Simba na Yanga ni kubwa na ni ngu­mu, na si kwa sababu nipo huku ndiyo niseme hivyo, hata nilivy­okuwa Yanga mechi hii tulikuwa tuki­ichukulia kwa umakini wa hali ya juu.

“Tunahitaji kujipanga ili tuweze kushinda mchezo huu, nime­jiandaa vizuri ili niweze kuisaid­ia timu yangu iweze kushinda.”

NADIR HAROUB ‘CANNA­VARO’

“Derby ya Simba na Yanga itakuwa nzuri na siku zote mchezo huu hauwezi kuutabiri, yeyo­te atakayefanya vizuri atashinda, tusubiri dakika 90.”

ABDALLAH SHAIBU ‘NINJA’

“Watu wanaoongea vibaya kuhusu mimi, basi wasubiri timu yao tutakapokutana Taifa, wasubiri kuona muz­iki wangu.”

Wachezaji wa timu ya Simba wakishangilia.

GADIEL MICHAEL

“Sina wasiwasi wowote na Simba kuelekea katika mchezo huu, kutokana na maandalizi makubwa tuliyoyafanya.

“Tupo katika maandalizi makubwa sana, naamini Sim­ba hawana pa kutokea, timu yetu ipo vizuri kupambana na timu yoyote kwa sasa na si Simba pekee.”

EMMANUEL OKWI

“Naamini wapinzani tukiku­tana nao tutawafunga mape­ma tu kutokana na kikosi chetu kukamilika kila idara, kwa maana kwamba kila mmoja wetu anatimiza maju­kumu yake ipasavyo.”

 

 

GEORGE LWANDAMINA

“Huku sisi tupo vizuri, tu­naendelea na mazoezi kama kawaida, kikubwa ambacho naweza kusema ni kwamba vi­jana wangu kila siku wanazidi kuwa imara na kunipa matu­maini ya kufanya vizuri dhidi ya Simba.

“Kwa namna siku zinavyozi­di kwenda, naona tupo tayari kwa mchezo huo, wapinzani wetu waje tu tupambane.”

JOSEPH OMOG

“Kwa sasa tupo tayari kwa ajili ya kucheza na Yanga kwa sababu kila ambacho nili­panga kukitoa kwa wachezaji kimekamilika na wamekishika kwa jinsi ambavyo nataka.

“Nikwambie tu kuwa hatuna presha na wapinzani wetu kwa sababu natambua tume­shacheza nao na tumepata matokeo mazuri mbele yao, imani yangu ni kwamba lazi­ma tutapata matokeo mazuri mbele ya wenzetu hao.”

Simba vs Yanga, Uwanja wa Taifa Hapatoshi, Sikiliza Tambo za Mashabiki


Stori: Khadija Mngwai | Championi Jumatano

 

Leave A Reply