The House of Favourite Newspapers

Tangazo La Kazi Halmashauri Ya Wilaya Karatu

0

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu anapenda kuwatangazia watanzania wenye sifa kuomba nafasi ya ajira ya kudumu na za Mkataba kwa kuzingatia maelezo ya kazi hapa chini:

NAFASI YA KAZI YA KUDUMU

DEREVA DARAJA LA II – NAFASI NNE (4)

a. Sifa za Mwombaji:
Mwombaji wa nafasi hii awe na ufaulu wa kidato cha nne
Awe na leseni daraja la “C” ya uendeshaji wa magari yote
Awe na Uzoefu wa kuendesha magari kwa muda usiopungua miaka mitatu bila kusababisha aiali
Awe mwenye cheti cha majaribio ya ufundi daraja la II (Grade test II) kutoka chuo cha usafirishaji (NIT) au chuo kinachotambulika na Serikali.

b. KAZI ZA KUFANYA
Kuendesha magari ya abiria na malori
Kuhakikisha gari na vyombo vyake vipo katika hali nzuri wakati wate.
Kufanya uchunguzi wa gari kabla na baada ya safari ili kubaini ubovu unaohitaji matengenezo
Kutunza na kuandika daftari la safari (Log book) kwa safari zote
Na kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa wake.

c. NGAZI YA MSHAHARA
Cheo hiki kina ngazi ya mshahara wa TGOS A, sawa Tshs. 300,000/- kwa mwezi bila nyongeza.

Katibu Muhtasi Daraja la III Nafasi moja (1)

a. Sifa za Mwombajl
Mwombaji awe na cheti cha ufaulu wa kidato cha nne
Awe amehudhuria mafuzo ya uhazili na kufaulu mitihani wa hatua ya tatu
Awe amefaulu somo la Hatimkato ya Kiswahili na Kingereza kwa maneno 80 kwa dakika moja.
Awe amepata mafunzo ya kompyuta kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali na kupata cheti katika programu ya Ms Publisher, Ms Excel. Ms Word, Power point, Internet na Email

b. NGAZI YA MSHAHARA:
Cheo hiki kina ngazi ya mshahara wa TGS B yaani Tsh. 390,000/- hadi 489,000 kwa mwezi.

c. KAZI ZA KUFANYA
Kuchapa barua, taarifa na nyaraka mbalimbali Kusaidia kupokea wageni na kuwasikiliza shida zao na kuwaelekeza sehemu wanapweza kuwasikilizwa. Kutunza tarifa/kumbukumbu za ofisi Na kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wake wa Kazi

NAFASI ZA KAZI YA MKATABA – MWAKA MMOJA (ONE YEAR)

d. MAELEKEZO YA JUMLA KWA WAOMBAJI KWA NAFASI ZOTE
Mwombaji awe ni Mtanzania
Mwombaji awe amehitimu kidato cha nne
Mwombaji awe na umri kati ya miaka 18 hadi 45
Mwombaji aambatanishe maombi yake na cheti cha kuzaliwa
Maombi yaambatane na sifa binafsi (CV), barua ya maombi, nakala za vyeti vya taaluma.
Testimonial, provisional results, statements of results, hati ya matokeo ya kidato cha nne au “che sita havitakubalika
Mwombaji aambatanishe maombi yake na picha mbili za hivi karibuni (passport size)
Maombi yote yatumwe ndani ya siku kumi (10) tangu tarehe ya tangazo hili

Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 05 mwezi 11 Mwaka 2017

MAOMBI VOTE YATUMWE KWA ANUANI IFUATAYO:

Mkurugenzi Mtendaji Wilaya,
S. L. P. 190,
Karatu.

Leave A Reply