Tanzania na Msumbiji Zatia Saini Mikataba ya Ulinzi na Usalama
Msumbiji na Tanzania Septemba 21, 2022 zimesaini mikataba miwili ya ushirikiano mjini Maputo inayolenga kupambana na ugaidi na uhalifu.
Msumbiji kwa sasa inapambana na wanamgambo wa Kiislamu katika eneo lenye utajiri wa gesi kaskazini mwa Cabo Delgado nchini humo.
Mikataba hiyo ilisainiwa ikiwa ni sehemu ya ziara rasmi ya siku tatu ambayo Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anafanya nchini Msumbiji.
”Katika kuhakikisha tunapambana na magaidi, kupitia mahusiano haya leo tumeweza kutia saini katika eneo la usalama na ulinzi, na hii ni hatua muhimu sana katika kusonga mbele” amesema rais Samia.
Mbali na kupambana na wanajihadi, Rais Filipe Nyusi alisema nchi hizo mbili kwa sasa zimejikita katika unyonyaji wa hidrokaboni ambayo ni nyenzo za ujenzi wa vyanzo muhimu vya nishati kama makaa ya mawe na gesi.
Rais Samia pia alisisitiza haja ya nchi zote mbili kuimarisha usalama kwa sababu ya mpaka wa pamoja wanaoshiriki.