TANZIA: Bongo Muvi Wapata Pigo, Aunt Fifi Afariki Dunia
Muigizaji wa filamu Bongo ambaye pia ni Diwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo kupitia Chama cha ACT Wazalendo, Tumaini Bigilimana maarufu kama Aunt Fifi, amefariki dunia hii jana, Jumatatu, Juni 4, 2019.

Taarifa juu ya kifo chake imetolewa na Kiongozi wa ACT Wazalendo Zitto Kabwe, na kueleza kwamba Bi. Tumaini amefariki dunia akiwa katika hospitali ya Rabininsia iliyopo Jijini Dar es Salaam.
Endelea kufuatilia mitandao yetu ya kijamii kwa taarifa zaidi juu ya msiba huu.


Comments are closed.