Kamanda wa polisi wa zamani mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Mohamed Chico amefariki dunia usiku wa kuamkia leo jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa msemaji wa familia Bw. Awadhi Chico, mazishi yake yamepangwa kufanyika leo Jumapili 22/01/2017 jioni katika Makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam. Msiba upo nyumbani kwa marehemu Kijitonyama. Habari ziwafikie ndugu, jamaa, marafiki na majirani popote pale walipo.
Mwenyezi Mungu amjaalie kauli thabiti na ailaze roho yake mahali pema peponi – AMINI
Comments are closed.