Picha za Viongozi wa Serikali na Wananchi wakifanya Usafi
leo nje ya jengo la Kibasila akiwamo Mwenyekiti wa Khoja Shia
Ithnashery Jamaat ya jijini Dar es Salaam, Dewji Azim (katikati). Kushoto ni Mwanasheria wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Veronica Hillary,
Mkuu wa Idara ya Upasuaji, Dk Julieth Magandi, Mkurugenzi wa Upasuaji,
Dk John Kimario na Mwenyekiti wa Khoja Shia Ithnashery Jamaat ya jijini
Dar es Salaam, Dewji Azim wakifanya usafi leo Desemba 9 ambayo ni siku
ya kuadhimisha Uhuru wa Tanzania. Usafi huo umefanyika katika Jengo la
Kibasila.
Mkurugenzi wa Upasuaji katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Dk John
Kimario akisomba takataka ikiwa ni sehemu ya kutekeleza agizo la Rais
John Pombe Magufuli kwamba leo Desemba 9, siku ya Uhuru watu wote
wajumuike kufanya usafi.
Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Huduma kwa Wateja, Aminiel Aligaesha (wa
pili kulia) akishiriki kufanya usafi katika hospitali hiyo leo Desemba
9, 2015.
Mkuu wa Idara ya Sheria, Veronica Hillary, Ofisa Uhusiano Msaidizi, John
Stephen, Mkurugenzi wa Upasuaji, Dk John Kimario na Mkuu wa Idara ya
Upasuaji, Dk Julieth Magandi wakijumuika pamoja kufanya usafi leo katika
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) ikiwa ni kuitikia agizo la Rais
John Pombe Magufuli la kufanya usafi leo Desemba 9, siku ya Uhuru.
Mwenyekiti wa Khoja Shia Ithnashery Jamaat ya jijini Dar es Salaam, Dewji Azim akifanya usafi leo katika hospitali hiyo.
Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Moses Nnauye akifanya usafi.Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo) akishirikiana na wananchi kufanya usafi kwenye Zahanati ya Rusimbi, Kigoma.Mchambuzi wa Masuala ya Siasa, Hamphrey Polepole akifanya usafi. Mitaa Mbalimbali ya Jiji la Mbeya imepokea vyema wito wa Rais
wa Awamu ya Tano juu ya agizo la kufanya Usafi Nchi nzima kwa
siku hii ya leo.Usafi ukiendelea katika Maeneo Mbalimbali ya Jiji
la Mbeya.
Wananchi mbalimbali wakifanya usafi.Usafi jijini Dar.
Wakazi wa Mbeya Mjini wakifanya usafi. Wakazi wa Mwanjelwa mkoani Mbeya wakitekeleza agizo la Rais magufli la kufanya usafi leo.