The House of Favourite Newspapers

Tatizo la nguvu za kiume, maana yake na tiba-3

0

blonde-woman-looking-at-unhappy-man-in-bedWiki iliyopita tuliangalia tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na tuliangalia utangulizi wa mada hii, leo ningependa kuendelea na vyanzo vinavyosababisha tatizo hilo.

Zifuatazo ni baadhi ya sababu zinazosababisha upungufu wa nguvu za kiume kwa wanaume walio wengi:

Kujichua kwa muda mrefu
Mtu anapojichua anakuwa anaiminya mishipa inayosababisha kusimama kwa uume, baada ya muda fulani, mishipa hiyo huishiwa nguvu na kulegea hivyo linapokuja suala la kusimamisha uume, mwanaume husika anakuwa hana uwezo tena wa kufanya hivyo.
λMadawa makali ya kuongeza nguvu za kiume

Madawa haya hasa yale ya kizungu husababisha mishipa ya uume kulegea kwa sababu unai-overdose mishipa hiyo na kuilazimisha kufanya kazi zaidi ya kiwango chake. Matumizi haya yanapokuwa ya muda mrefu humfanya muhusika kuwa tegemezi na pia hufanya mishipa yake ya uume kulegea na kukosa nguvu.

Ulaji wa vyakula vya mafuta kwa wingi
Hii nayo husababisha kuathiri moyo na mzunguko wa damu mwilini na hivyo uume kukosa msukumo wa damu wa kutosha katika mishipa yake.
Presha na ugonjwa wa kisukari
Uoga au wasiwasi wa kufanya tendo la ndoa
Ulevi kupita kiasi

Mfano ulevi kupita kiasi wa pombe, madawa ya kulevya husababisha mwanaume kupoteza nguvu za kiume. Msomaji ningependa kukujulisha kuwa tafiti zinaonesha unywaji pombe unaathari nyingi katika afya ya binadamu, husababisha tatizo la kuharibika kwa ini (Liver damage), uharibifu wa mfumo wa fahamu (Nervous system) na kuvuruga mpangilio wa uzalishaji wa tezi za uzazi wa kiume na hatimaye kusababisha upungufu wa nguvu za kiume.

Usikose kufuatilia mada hii Alhamisi ijayo kwenye gazeti hilihili.

Leave A Reply