The House of Favourite Newspapers
gunners X

Global T V Online Ilivyoendesha Mjadala Live Kuhusu Sakata la Madawa ya Kulevya Nchini

CHANNEL PENDWA YA GLOBAL TV ONLINE leo imefanya mjadala mubashara kuhusu sakata la madawa ya  Wahariri na waandishi wa Global Publishers wamechangia kwa kina kuhusu mjadala huo na haya ndiyo yalikuwa maoni yao.

 

Wajume wakichangia majadiliano.

Mjadala umeanza, mhariri kiongozi, Oscar Ndauka anazungumza

Ndauka amekumbushia ishu ya Amina Chifupa alivyopoteza maisha baada ya kusema angewataja majina wauza madawa.

Una chochote cha kuzungumza kuchangia mjadala huu? Weka maoni yako.

Phillip Nkini, Mhariri Championi anazungumza.

Nkini: Ni kweli kuna tattoo la madawa ya kulevya lakini utaratibu unaotumika siyo sahihi, ukimtaja mtu mapema kabla ya kumquat na vidhibiti, anaweza kuvuruga ushahidi.

Nkini: Naunga mkono vita ya madawa lakin mbinu ibadilishwe, Watanzania wote tuungane bila kujali itikadi

 

 

Lawrence Kabende, mhasibu mkuu anazungumza

Kabende: Makonde amethubutu kujiweka hadharani na kuhatarisha maisha yake.

Erick Evarist, mhariri Risasi Jumamosi anazungumza

Evarist: Watuhumiwa wangechunguzwa kimyakimya kwanza, wakipatwa na hatia ndiyo watangazwe

Una nini cha kuchangia? Toa mano yako

Imelda Mtema, mwandishi mwandamizi anazungumza

Imelda: Lazima jamii nzima ishiriki kikamilifu, uchunguzi zaidi ufanyike mahali wanaposhinda mateja na wabanwe waoneshe wanaponunua madawa.

John Joseph, mhariri Championi anazungumza.

John: Naunga mkono vita lakini siungi mkono aproach

Emanuel, mwanasheria wa Global anazungumza sasa

Emanuel: Ni ukwell usiopingika kwamba athari za madawa zinatuathiri sote lakini lazima sheria izingatiwe kuwashughulikia wahusika.

Mhariri Mteandaji wa Global Publishers, Saleh Ally akichangia mada.

Emanuel: Kumtaja mtu kuhusika na madawa, siyo kosa kisheria kwa sababu mtuhumiwa ana nafasi ya kujitetea na mahakama ndiyo itatoa jibu la mwisho
Sifael Paul, mhariri wa Ijumaa Wikienda anazungumza.
Sifael: Kumkamata mtu bila kuwa na proof ni makosa, hii vita ni kubwa na ya kimataifa lakini kwa jinsi hali ilivyo sasa, wakamatwe tu hata bila proof, tuache unafiki.
Bahati Haule, msanifu kurasa mkuu anazungumza.
Bahati: Tumuombee Makonda
Gabriel Ng’osha, mwandishi wa habari anazungumza
Ng’osha: Watanzania tuache unafiki, tumuunge mkono Makonda
Ndugu mtazamaji, maon yako ni ya muhimu sana

Boniface Ngumije, mwandishi wa habari anazungumza

Ngumije: Namshauri Makonda hii vita aiishie njiani, ahakikishe inafika mwisho.
Amran Kaima, mhariri Ijumaa anazungumza
Ojuku Abraham, Mhariri Risasi anazungumza
Ojuku: Rais wa Panama alikuwa anahusika na biashara ya madawa, Marekani wakaenda kumkamata, kumtaja mtu siyo tatizo naunga mkono vita lakini sheria ya namna ya kuwakamata ifuatw
Ezekiel Kitula, Mhariri Championi anazungumza

Sales Ally, Mhariri Mtendaji anazungumza.

Saleh: Simuungi mkono makonda kuwataja watu bila kuwa na ushahidi
​Mkurugenzi Mtendaji wa Global Publishers, Eric Shigongo akichangia mada wakati wa mjadala huo.
Eric Shigongo, Mkurugenzi Mtendaji wa Global anazungumza sasa.
Shigongo: Kama taifa tupo vitani, tuungane na tupambane kwa pamoja
Shigongo: Kwenye vita ya madawa ya kulevya isiwe kwa ajili ya watu kutaka sifa
Shigongo: Rais Magufuli atusaidie kuhakikisha madawa hayaingii nchini, atumie mamlaka yake

Shigongo: Serikali iwasaidie vijana kutengeneza ajira kwa kujiajiri wenyewe, wazazi wawajibike

Mjadala umehitimishwa

Ahsanteni kwa kushiriki, na mpaka hapa tumefika mwisho

PICHA ZOTE NA MUSA MATEJA | GLOBAL PUBLISHERS

Comments are closed.