The House of Favourite Newspapers

TCRA Yatoa Mwongozo Wa Kurusha Matangazo Mubashara

0

Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA) imesema, Vituo vya Utangazaji ambavyo vitarusha matangazo mubashara vinaelekezwa kufuata mwongozo ili kuwa na ufanisi katika usimamizi na ufuatiliaji wake.

 

Imesema, kituo kitakachorusha matangazo mubashara kama vile Sherehe za Kitaifa ambazo ziko kwenye kalenda kinapaswa kutoa taarifa siku 14 kabla. Taarifa hiyo itaeleza mahali, muda wa kuanza na kumaliza tukio (kama unafahamika).

 

Vilevile, Kituo kitakachorusha matangazo mubashara ya dharura, kiifahamishe Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa kutumia barua pepe na kubainisha; aina ya tukio na mahali litakapofanyika, muda wa kuanza na kumaliza(kama unafahamika).

Leave A Reply