The House of Favourite Newspapers

TFF haijui lini itatumia tiketi za kielektroniki

0

Jamal-MalinziBAADA ya kelele nyingi kutoka kwa wadau wa soka, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limesema haina shida watarejesha matumizi ya tiketi za kielektroniki lakini halijui lini zitaanza kutumika.

Wadau mbalimbali wa soka kwa muda mrefu wanailaumu TFF kwa kuacha kutumia mfumo wa tiketi za kielektroniki kuingia katika viwanja vinavyotumiwa kwa mechi za Ligi Kuu Bara.

Wakati inasitisha matumizi ya tiketi hizo, TFF ilisema ilikuwa inakumbana na tatizo la miundo mbinu kutoendana na mfumo wa tiketi hizo ikiwa ni pamoja na uhaba wa milango katika baadhi ya viwanja.

Katibu Mkuu wa TFF, Selestine Mwesigwa, ameliambia Championi Jumamosi kuwa, wapo kwenye mchakato wa kuhakikisha wanaurejesha tena utaratibu huo msimu huu, lakini bado haijajulikana utaanza lini.

“Tupo kwenye mchakato wa kutatua zile changamoto zilizojitokeza wakati wa matumizi ya tiketi za elektroniki, tunapambana kuhakikisha tunaurudisha kwa kuwa sasa tumesimama kwa muda,” alisema Mwesigwa.

“Siwezi kusema utaanza lini na katika mechi ipi, lakini ndipo tunakoelekea kwenye msimu huu ili tuachane na mfumo huu wa sasa.”

Pia mfumo huo wa tiketi uliokuwa unatumika kwa ushirikiano na Benki ya CRDB, ulikumbwa na changamoto nyingine ya uchache wa mashine za kuchapa na kuhakiki tiketi hizo uwanjani.

JIUNGE NA MICHEZO KIGANJANI TUMA NENO SPORTS KWENDA NAMBA 15778CHAMPIONI

Leave A Reply