The House of Favourite Newspapers

TIGO YANG’ARISHA MKUTANO WA MAWAZIRI WA SADC

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe  akisajili upya laini yake ya simu kwa mfumo wa alama za vidole  alipotembelea banda la Tigo wakati wa mkutano wa mawaziri kuhusu Teknolojia ya Habari na Mawasiliano  (Tehama) wa nchi wanachama wa Jumuia ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) unaoendelea jijini Dar es Salaam. Kampuni ya simu ya Tigo ni mtoa huduma ya WI-FI ya bure katika wa mkutano huo.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji (TBC) Ayub Rioba akisajili laini yake ya simu kwa mfumo huo pia.
Mtaalamu wa Tehama, Benjamin Sabuka,  akipata maelekezo kutoka kwa mfanyakazi wa kampuni ya Tigo juu ya huduma zitolewazo na kampuni hiyo.
Kamwelwe akipata maelezo mbalimbali  ya huduma za Tigo kutoka kwa mfanyakazi wa kampuni hiyo. 

NCHI za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), zipo katika mkakati wa kuwa na mfumo satelaiti ambao utawezesha taarifa za nchi hizo kudhibitiwa katika ukanda huo bila kuvuka mipaka.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhandisi Isack Kamwelwe,  wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mawaziri wa SADC wa Sekta ya TEHAMA, Habari, Uchukuzi na Hali ya Hewa waliokutana jijini Dar es Salaam.

Kamwelwe ameema kwa muda mrefu nchi za SADC zimekuwa zikitumia mfumo wa satelaiti ambao unahitaji taarifa kwenda katika nchi za Ulaya na Marekani ndipo zirudi nchini na kumfikia mhusika,  hivyo wanataka kuondokana na utaratibu huo.

 

Comments are closed.