Timu ya Mpira wa Pete ya OSHA Yatwaa Ubingwa Daraja la Tatu na Kupanda Daraja la Pili
Kikosi cha mpira wa pete cha Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA Netball Club) kimetwaa ubingwa wa mashindano ya mpira wa pete ngazi ya Ligi Daraja la Tatu na hivyo kupanda Ligi Daraja la Pili.
Mashindano hayo ya ligi daraja la tatu Mkoa wa Dar es Salaam yaliyofanyika katika viwanja vya TBS vilivyopo Ubungo Dar Es Salaam, yalishirikisha timu sita Timu zikiwemo: TBS, COMFORT, OSHA, BENJAMINI MKAPA S.S, DAR ZONE COMBINE NA MAKONGO SPORT ACADEMY.
Sambamba na hayo pia ametoa ombi kwa Mtendaji Mkuu wa OSHA kuendelea kuilea na kuiwezesha timu hiyo iweze kufika mbali kwa kuendelea kutwaa ubingwa wa michuano mbalimbali itakayo shiriki.
Kwa upande wake nahodha wa timu ya OSHA, Bi. Rachel Nkoma ametoa pongezi kwa wachezaji wote, viongozi wa taasisi wakiongozwa na Mtendaji Mkuu wa OSHA kwa jitihada walizofanya kuiwezesha timu kutwaa ubingwa.
Timu ya OSHA ilishinda michezo yote mitano ambapo mechi ya kwanza iliifunga timu ya TBS kwa vikapu 44 kwa 20. Mechi ya pili ilikuwa dhidi ya Benjamini Mkapa ambapo OSHA ilishinda kwa jumla ya Vikapu 43 kwa 27. Matokeo ya michezo mingine yalikuwa kama ifuatavyo: OSHA dhidi ya Dar Zone (vikapu 52 kwa 37), OSHA dhidi ya Comfort (44 kwa 41) na OSHA dhidi ya Makongo (vikapu 61 kwa 7).