The House of Favourite Newspapers

TMA Yatabiri Mvua, Upepo Mkali

0

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania imesema kesho Mei 4 kuna uwezekano wa uwepo wa upepo mkali unaokadiriwa kufikia kilometa 40 kwa saa, uwepo wa mawimbi makubwa yanayofikia mita 2 katika baadhi ya maeneo ya ukanda wa Pwani wa Bahari ya Hindi.

 

MATARAJIO YA MWENENDO WA MVUA KWA SIKU 10 ZIJAZO KUANZIA TAREHE 01- 10 MEI 2021.

Kanda ya ziwa Victoria (Mikoa ya Kagera, Geita, Shinyanga, Mwanza, Simiyu na Mara): Vipindi vya mvua vitakavyoambatana na ngurumo za radi katika baadhi ya maeneo.

 

Nyanda za juu kaskazini-mashariki (Mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro,): Vipindi vya mvua vitakavyoambatana na ngurumo za radi katika maeneo machache.

 

Pwani ya kaskazini (Mikoa ya Tanga, Maeneo ya kaskazini mwa Morogoro, Pwani na Dar es Salaam pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba): Vipindi vya mvua vitakavyoambatana na ngurumo za radi katika baadhi ya maeneo.

 

Magharibi mwa nchi (Mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora): Vipindi vya mvua zitakazoambatana na ngurumo za radi katika maeneo machache.

 

Kanda ya kati (Mikoa ya Dodoma na Singida): Vipindi vya mvua nyepesi katika maeneo machache.

 

Nyanda za juu Kusini-magharibi (Mikoa ya Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Iringa): Vipindi vya mvua nyepesi katika maeneo machache.

 

Pwani ya kusini (Mikoa ya Mtwara na Lindi): Vipindi vya mvua nyepesi katika maeneo machache. Kanda ya kusini (Mkoa wa Ruvuma na Maeneo ya kusini mwa Morogoro): Vipindi vya mvua nyepesi katika maeneo machache.

Leave A Reply