RAIS Donald Trump amekubali kuanza kwa mchakato rasmi wa kumkabidhi madaraka Rais Mteule Joe Biden kwa kuliambia shirika linaloshughulikia mabadilishano hayo “lifanye kile kinachostahili kufanywa” hata wakati anaahidi kuendelea kupinga matokeo.
Ofisi ya utawala wa huduma za serikali imesema inamtambua Biden kama “mshindi”. Hilo linawadia wakati Biden ameidhinishwa rasmi kama mshindi wa jimbo la Michigan na kuwa pigo kubwa kwa Trump.
Timu ya Biden imefurahishwa na kuanza kwa mchakato huo wakati Rais Mteule anajiandaa kwa sherehe za kuapishwa Januari 20.