The House of Favourite Newspapers

Trump Amtuhumu Obama Kuhusika na Maandamano Yanayoendelea Marekani

MAREKANI: Rais wa Marekani, Donald Trump amesema anaamini kuwa Rais Mstaafu wa Nchi hiyo, Barack Obama ndiye anahusika na maandamano dhidi ya uongozi wa Republican.

“Nafikiri Rais Obama anahusika kwa sababu ni watu wake wanaohusika kwenye maandamano hayo,” Trump alikiambia kituo cha Fox News.

Trump hakutoa ushahidi wowote kwa madai yake, waati huo Rais Obama bado hajajibu lolote kuhusu tuhuma hizo.

Trump pia alizungumzia bajeti na masuala mengine huku akieleza kuwa, amepanga kuongeza bajeti kwa ajili ya Jeshi la Ulinzi la nchi hiyo.

Comments are closed.