Awali taarifa zilisambaa mitandaoni kuwa waziri huyo amekamatwa na polisi kwa mahojiano, jambo ambalo Makamba amekanusha.
“Sijakamatwa na polisi. Niko salama,” ameandika Makamba kupitia ukurasa wake wa Twitter.
Baadaye akafafanua…
Alichokiandika Makamba siku ya tukio la kutekwa kwa Mohammed Dewji.
Makamba ni miongoni mwa watu waliopata taarifa mapema za kupatikana kwa bilionea huyo na kuandika katika mtandao wa kijamii wa Twitter.
Mo Dewji alitekwa Oktoba 11, 2018 katika Hoteli ya Colosseum alikokwenda kwa ajili ya kufanya mazoezi na kupatikana Oktoba 20 saa nane usiku, baada ya waliomteka kumtelekeza katika viwanja vya Gymkhana, jijini Dar es Salaam.
Comments are closed.