The House of Favourite Newspapers

Tunda Afungukia Mimba Ya Mbongo Fleva

0

 

Tunda Sebastian

BAADA ya habari kuzagaa kwamba mrembo anayeuza nyago kwenye video mbalimbali Bongo, Tunda Sebastian kuwa na ujauzito wa staa wa Bongo Fleva, ameibuka na kufungukia ishu hiyo.

 

Tunda Sebastian akifanya yake na Young Dee.

Akizungumza na Star Mix, Tunda alisema hana ujauzito wa msanii huyo kama watu wasemavyo na kwamba huwa
anamuweka katika mitandao ya kijamii husan Instagram kwa sababu ya kumsapoti katika kazi zake.

 

“Ndiyo kwanza nasikia kwenu, siyo kweli na sina mimba yake. Huwa namuweka Insta kumsapoti kikazi tu maana ni rafiki yangu sana lakini watu walivyoona hivyo wakaanza kuzusha maneno hayo kwamba ninatoka naye na nina mimba yake. “Kuhusu kunenepa, nimenenepa kwa sababu nimeridhika na maisha mazuri niliyo nayo,” alisema Tunda.

STORI: IMELDA MTEMA

Usipitwe na Matukio, Install App Yako ya Kijanja na Namba Moja Tanzania ya Global Publishers

Android ===>Google Play

iOS ===>Apple Store

Leave A Reply