The House of Favourite Newspapers

Lissu: Bado Sijapokea Wito wa Malalamiko NEC

0

MGOMBEA urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, amesema kuwa hadi sasa bado hajapokea wito wala malalamiko yoyote kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwa mujibu wa taarifa ya tume hiyo ilivyoeleza hapo jana.

 

Lissu ametoa kauli hiyo hii leo Septemba 30, 2020, wakati akizungumza na waandishi wa habari mkoani Arusha, na kusisitiza kuwa kwa sababu hana wito wowote yeye ataendelea na ratiba zake za kampeni kama ilivyo kwenye ratiba.

 

Jana Septemba 29, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC Dkt. Wilson Mahera, alitoa taarifa ya kuthibitisha kumwandikia barua ya wito Tundu Lissu, kufuatia tuhuma mbalimbali anazodaiwa kuzitoa kati ya Septemba 25 na 26 mjini Musoma.

Leave A Reply