The House of Favourite Newspapers
gunners X

WASHINDI WA DROO YA SABA NA NANE WAKABIDHIWA ZAWADI

Ezbon Bwire, mwakilishi wa Jackson Bwire wa Ukerewe, Mwanza, akiwa amekaa juu ya pikipiki baada ya kukabidhiwa.

Hatimaye washindi wa droo ya saba na nane kwenye Shindano la Tusua Maisha na Global, leo wamekabidhiwa zawadi zao walizojishindia, tukio lililofanyika katika Ofisi za Global Publishers, Sinza Mori jijini Dar es Salaam.

Aziz Hashim (kulia), mwakilishi wa kampuni ya Global Publishers akizungumza jambo wakati wa kukabidhi zawadi kwa washindi. Pembeni yake ni Glory Lucas kutoka idara ya uhasibu.

Waliokabidhiwa zawadi zao leo ni Said Katambo wa Nachingwea, Lindi aliyefunga safari mpaka jijini Dar es Salaam kufuata zawadi yake ya pikipiki, na Ezbon Bwire aliyemwakilisha ndugu yake, Jackson Bwire wa Ukerewe ambaye pia amejishindia pikipiki.

Said Katambo (kushoto), akikabidhiwa kadi ya pikipiki aliyoshinda na John Joseph, Mwakilishi wa Kampuni ya SokaBet.

Wengine waliokabidhiwa zawadi zao ni Benard Kapembe aliyejishindia headphones na Boniphace Malick wa Bunju aliyejishindia dinner set.

Washindi wengine ambao zawadi zao zitatumwa kwa wawakilishi wetu wa mikoani, Nobert Benjamin wa Nyamagana, Mwanza aliyejishindia dinner set, Gasper Ndimbo wa Mkuranga aliyejishindia jezi na Ally Bakari wa Vikindu aliyejishindia jezi.

Boniphace Malick (kushoto) wa Bunju, akikabidhiwa zawadi ya dinner set na Jimmy Haroub, Afisa Masoko wa GPL.

Wakati huohuo, washindi wa droo ya tisa wamepatikana katika droo iliyochezeshwa Ijumaa ambapo Simba Ramadhan, mkazi wa Mbezi jijini Dar es Salaam ameibuka mshindi wa pikipiki mpya huku Anna Mbise, mfanyabiashara kutoka Arusha akijishindia dinner set na Hussein Mtipa wa Ifakara, Morogoro akijishindia jezi.

Boniphace Malick akizungumza baada ya kukabidhiwa zawadi.

Ili kuwa miongoni mwa washindi, nunua gazeti lolote linalochapishwa na Global Publishers kati ya Uwazi, Risasi, Amani, Ijumaa, Ijumaa Wikienda, Championi na Spoti Xtra kisha funua ukurasa wa pili ambapo utakutana na kuponi yenye maelekezo ya namna ya kushiriki.

Benard Kapembe (kushoto) akikabidhiwa zawadi ya head phones na Given Mashishanga wa Global TV.

Itume namba maalumu inayoonekana juu ya kuponi kwa njia ya meseji kwenda namba 0719386533. Hakikisha unahifadhi kuponi au gazeti lako kwani linahitajika wakati wa kuchukulia zawadi vigezo na masharti vinazigatiwa.

Ezbon Bwire (kushoto) akikabidhiwa kadi ya pikipiki na Glory Lucas wa Idara ya Uhasibu GPL.
Washindi wakiwa katika picha ya pamoja
Said Katambo akitesti mtambo wake

(PICHA: RICHARD BUKOS | GPL)

Comments are closed.