The House of Favourite Newspapers

Uamuzi Wabunge Waliofukuzwa CUF Agosti 25

0
Wabunge waliofukuzwa CUF wakiwa kortini.

MHAKAMA Kuu imeahirisha kutoa hukumu juu ya pingamizi lililowasilishwa na wabunge wanane  wa Viti Maalum wa CUF kupinga Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwaapisha wabunge wapya walioteuliwa na Mwenyekiti wa chama hicho anayetambuliwa na Msajili wa Vyama,  Prof. Ibrahim Lipumba.

 

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Mawasiliano  anayeunga mkono upande wa Maalim Seif, Mbarala Maharagande, kesi hiyo imeahirishwa hadi  Agosti 25 mwaka huu itakapotoa uamuzi kuhusu suala hilo.

 

Maharagande aliyasema hayo alipoongea na waandishi wa habari baada ya kutoka  nje ya mahakama hiyo.

NA DENIS MTIMA | GPL

=========

VIDEO KILICHOJIRI KORTINI

Leave A Reply