Uchaguzi Kenya: Mgombea Urais Kupitia Azimio, Raila Odinga Afanikiwa Kumpita William Ruto
Mgombea Urais kupitia Azimio, Raila Odinga amefanikiwa kumpita William Ruto kwa idadi ya Kura baada ya kuwa nyuma kwa Saa kadhaa
Hadi kufikia leo saa 6:30 mchana Odinga alikuwa na kura 6,431,752 (49.46) akifuatiwa na William Ruto mwenye Kura 6,389,957 (49.14%)
Prof. Wajackoyah Kura 56,430 (0.43%) na Mchungaji David Waihiga alikuwa na Kura 28,973 (0.22%). Kwa mujibu wa Citizen mpaka sasa jumla ya Kura 12,907,112 kati ya Milioni 14 zimehesabiwa.