The House of Favourite Newspapers

Ufaransa Mabingwa wa Kombe la Dunia – Video

TIMU ya Taifa ya Ufaransa imefanikiwa kunyakua Ubingwa wa Dunia mwaka 2018 baada ya kuifunga Croatia kwa bao 4-2.

 

Mabao ya Ufaransa yamewekwa kimiani na Mario Mandzukic aliyejifunga, Antoine Griezmann aliyefunga kwa njia ya penati pamoja, Paul Pobga pamoja na Kylian Mpabbe.

Wakati huo mabao ya Croatia yamepachikwa kimiani na Ivan Perisic pamoja na Mario Mandzukic aliyesahihisha makosa yake kwa kuifungia timu yake bao la pili.

Ubingwa huo kwa Ufaransa unakuwa wa pili baada ya kuutwaa pia katika mashindano ya Kombe la Dunia mwaka 1998 nchini kwao.

Kocha wa timu hiyo, Didier Deschamps amekuwa miongoni mwa makocha watatu kutwaa ubingwa huo kama mchezaji na Kocha baada ya Mbrazil Mario Zagallo na Mjerumani Franz Beckenbauer.
Vilevile Ufaransa imekuwa timu ya kwanza kufunga mabao manne katika fainali hizo tangu Brazil iifunge Italia 4-1 mwaka 1970.

 

Mario Mandzukic (bao la kujifunga) 18′,
Ivan Perisic (bao la kusawadhisha) 28′
Antoine Griezmann 38′
Paul Pogba 59′
Kylian Mbappe 69′.
Mario Mandzukic ni mchezaji wa pili kwenye historia ya kombe la dunia kuifungia goli timu yake na kujifunga kwenye mchezo mmoja baada ya Ernie Brandts kufanya hivyo mwaka 1978 kwenye mchezo wa nchi yake (Uholanzi) dhidi ya Italia.
Mbappe anaandika Historia baada ya kuibuka mchezaji Bora Chipukizi akiwa na umi mdogo lakini akifanya maajabu makubwa kwa kumaliza michuano hiyo akiwa na mabao 4 na Luka Modric (32) akiibuka mchezaji Bora wa mashindano hayo na kuondoka na kiatu cha dhahabu.
Kylian Mbappe anakuwa mchezaji wa pili mdogo kufunga goli kwenye mchezo wa fainali ya kombe la dunia baada ya Pele kufunga goli kwenye fainali ya mwaka 1958 akiwa na miaka 17 na siku 249, Mbappe ana miaka 19 na siku 207.

Comments are closed.