The House of Favourite Newspapers

Uhuru Kenyatta Amwandikia Barua Rais Magufuli

Rais Magufuli akiteta jambo na Rais Uhuru Kenyatta.

RAIS Uhuru Kenyatta wa Kenya amemuandikia barua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, kupinga kitendo cha mauaji ya askari wake 15 waliokuwa wakilinda amani nchini Kongo, na kumpa pole kufuatia msiba huo mkubwa.

 

Katika barua hiyo, Rais Kenyatta amesema kushambuliwa kwa askari, ambao walikuwa wakihudumia kwa sababu nzuri ya kuanzisha amani ya kudumu nchini DRC ilikuwa mbaya, huku akiwapa pole watanzania na ndugu wa marehemu, na kuwaombea wale waliojeruhiwa waweze kupona haraka.

 

Uhuru Kenyatta ameendelea kwa kusema kwamba Kenya itaendelea kushirikiana na watu na serikali ya Tanzania katika kulinda amani ya Kongo na maeneo ya maziwa makuu, na kuangalia kesho bora ya maeneo hayo.

 

Rais Kenyatta amesema Kenya inathamini jukumu muhimu lililofanywa na watunza amani tangu imehusika katika mipango mingi ya kulinda amani.

 

Mwishoni mwa wiki iliyopita askari 15 wa Tanzania waliokuwa wakilinda amani nchini Kongo waliuawa na askari waasi wanaoendesha ampigano nchini humo, huku 44 wakijeruhiwa, 8 wakiwa mahututi na wawili hawajulikani walipo.

VIDEO YA MATOKEO HAYO IKO HAPA

Comments are closed.