The House of Favourite Newspapers

Ujauzito Wampeleka Puta Kadijanito

0
Kadja Nito.

 

MTOTO mzuri kwenye Bongo Fleva, Natasha Lisimo ‘Kadja Nito’ amekiri kupelekwa puta na ujauzito aliona ikiwemo kuwachukia baadhi ya watu wake wa karibu.

 

Akibonga na Showbiz Xtra, Kadja Nito alisema kuwa, kwa sasa amelazimika kuhama alikokuwa akiishi awali maeneo ya Mwenge, Dar na kwenda kuishi Kurasini ili kuwa mbali na watu ambao anahisi ataendelea kuwakwaza kwa jinsi mimba hiyo inavyompelekesha.

 

“Nimejikuta sipendi kuonana na watu wengi ninaowajua, ndiyo maana nimeamua kuhamia Kurasini ili niwe mbali na karaha inayonipata. Unajua mimba zinasumbuaga sana, lakini jamaa zangu wanivumilie tu,” alisema msanii huyo mwenye ujauzito wa miezi kadhaa alioupata baada ya kuolewa.

 

Mzee Majuto Awajibu Waliomzushia Kifo, Tazama Video Hii

Leave A Reply